20% akamilisha Party yake New Msasani
Abasi Kinzasa aka 20% Mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya ambaye ameshangaza watu kwa kujinyakulia tuzo tano kwa nyimbo mbili, katika kinyanyiro cha Kili Music Award. hii ilikuwa ni moja ya Party yake iliyofanyika pale New Msasani karibu na ubalozi wa Marekani April 15, kuwashukuru mashabiki wake kwa kumpigia kura.
Mwanamuziki huyo aliweza kuwaonyesha pia kwamba hayupo ‘Fit’ katika kuimbaji na kutunga tu, bali kila kona hata katika mambo ya ‘Perfomance’ jukwaani yaani anakimbiza. Pi aliweza kuimba wimbo amabao ulikutanisha wasanii wote ambao walikuja eneo hilo, hakika ilikuwa burudani zaidi, kwa video zaidi ya usiku huo ingia kwenye Bongo5 video ujionee.
Mkali mwingine toka Arusha ama ukipenda unaweza kupaita A-Town, anaitwa Stopper na nyimbo yake mtu 3 ndani ya staili moja.
Mwanamuziki PNC aliyetamba kipindi kileee, naye alikuwepo lakini zaidi alikuwepo pamoja na Ney wa Mitego katika jukwaa moja, hakika ilikuwa ni usiku wa kuvutia kwa mashabiki.
Man water akaamua mzingo ausimamie mwenyewe…………………….