Siasa
20% apata mialiko na viongozi wa juu
Mwanamuziki Twenty Percent aka Abbas Kizansa, amesema amefurahia sana kupata tuzo tano katika kinyang’anyiro cha Kilimanjaro Music Award na kusema sasa ametiwa moyo kwa kazi anayoifanya, na kutimiza lengo lake alilokuwa analifikiria kila siku.
Amesema sasa lengo lake ni kumiliki bendi, ambayo atakuwa akipiga na kundi lake la Form Boys, ili kuleta ladha tofauti, na kuonyesha ujuzi wake wa kutumia gitaa.
Aidha alidai tuzo ilimpelekea kupata mialiko sehemu mbalimbali, ikiwemo serikalini kwa wazilri wa Nishati na madini, MH. Lowasa na Mtoto wa raisi, Ridhwan Kikwete.
Anasema wapo waliomiuahidi, na wengine kumpongeza kwa kazi nzuri, hata hivyo wasanii wenzake pia wamekuwa mstari wa mbele katika kumpongeza kwa kumfanyia sherehe mbalimbali kama kumpongeza na kumfariji katika kazi zake.
Moja ya party wakimpongeza Twenty kwa kupokea tuzo tano kwa nyimbo mbili.