Michezo
Tiketi za kombe la dunia 2018 zaanza kuuzwa
Kuelekea michuano ya fainali ya kombe la dunia nchini Urusi hapo mwakani tayari tiketi za awali zimeanza kuuzwa hapo jana siku ya Alhamisi.
Mashabiki sasa wataweza kuwasilisha maombi yao kupitia tovuti ya Shirikisho la Mpira wa Miguu duniani ‘FIFA’ na tiketi zitauzwa kwa awamu mbili.
soma zaidi – Gharama za tiketi za kombe la Dunia zatajwa
Mchakato wa uuzwaji wa tiketi hizo umeanza hapo jana majira ya saa 6 mchana kwa saa za Urusi ambazo ni sawa na saa za Afrika Mashariki.
Unaweza kununua tiketi yako HAPA