Burudani

Cardi B atangaza ujio wa albamu yake mpya, inatoka mwezi …

Je unatamani kuisikia albamu ya Cardi B? Rapper huyo wa kike mwenye kasi ya 4G kwenye muziki, ametangaza ujio wa albamu yake mpya ambayo itatoka mwezi ujao.

Mrembo huyo amethibitisha hilo usiku wa Jumapili hii wakati wa sherehe za utoaji tuzo za iHeartRadio Music Awards 2018 mjini Los Angeles.

“My album will be coming in April, okurr!. Yes, sir, April. Stay tuned, motherfu**ers,” amesema Cardi B wakati akipokea tuzo yake ya msanii bora chipukizi.

Miongoni mwa ngoma ambazo zinatarajiwa kusikika katika albamu yake hiyo ya kwanza ni pamoja na Bodak Yellow (Money Moves) na ‘Bartier Cardi’.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents