Mahojiano

Nyandutoz aweka wazi kuhusu kusainiwa WCB na Diamond “Nikiwa chini yao nakuwa na amani sana” – Video

Nyandutoz aweka wazi kuhusu kusainiwa WCB na Diamond "Nikiwa chini yao nakuwa na amani sana" - Video

Msanii wa muziki wa Bongo Fleva Rapper Nyandutoz ameweka wazi kuhusu ukaribu wake na Diamond Platnumz baada ya kusemekana ndio msanii anayetarajiwa kusainiwa katika lebo iliyochini ya Diamond.

Mbali na habari hizo kusikika pia ikumbukwe kuwa Nyandu alitangaza kuwa kwa mwaka huu 2020 anatarajia kuwa chini ya usimamizi wa lebo moja ya muziki hapa Tanzania.

Nyandutoz tangua aanze muziki hajawahi kuwa chini ya lebo wala menejimenti yeyote zaidi ya yeye na Mr Blue kuanzia B.O.B MICHARAZO ambapo yeye alikuwa muanzilishi wa B.O.B na Mr Blue akianzisha MICHARAZO lakini waliamua kuziunganisha na kuwa B.O.B MICHARAZO hadi kufikia muda kuwa na baadhi ya wasanii waliokuwa wanaunda kundi hilo ingawa walikuja kugawanyika.

Mbali na hilo Nyandutoz ameeleza kuhusu historia ya maisha yake na kufunguka kuhusu kuhusika katika video ya wimbo wa Diamond wa KANYAGA.

By Ally Juma.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents