Michezo
AC Milan ya uzwa kwa wa China
Kampuni ya China, Rossoneri Sport Investment Lux imekamilisha rasmi ununuzi wa klabu ya AC Milan ya Italia kutoka kwa Silvio Berlusconi kwa Euro milioni 740.
Klabu hiyo ya Serie A imekuwa chini ya umiliki wa bilionea Silvio Berlusconi, tangu mwaka 1986.
Katika kipindi hicho chote, AC Milan ilifaulu kunyakua mataji manane katika ligi kuu na kunyakuwa kombe la vilabu bingwa barani Ulaya mara tano.
Kwa sasa inashikilia nafasi ya 6 katika ligi kuu, alama 20 nyuma ya vinara Juventus.