HabariUncategorized
ACT wafunguka ishu ya Mhe. Zitto kufichwa, kutishiwa kuuawa na usalama wake kwa sasa (+video)
Chama cha ACT Wazalendo kimeweka wazi kuwa kiongozi wao Mhe. Zitto Kabwe amepata vitisho kutoka kwa watu wasiojulikana wakitishia usalama wake.
Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Aprili 24, 208 katika Ofisi Kuu za Chama hicho jijini Dar es salaam, Katibu Itikadi na Uenezi, Ado Shaibu amesema kuwa kiongozi huyo hajafichwa kama watu wengi wanavyozusha na tayari wameshamuandikia barua IGP Sirro, kutaka uchunguzi ufanyike na ulinzi uimarishwe kwa kiongozi huyo kwani ni jukumu la Jeshi la polisi kulinda raia wake.