Habari
ACT Wazalendo watuma barua kwa IGP Sirro
Chama cha ACT Wazalendo kimesema kuwa tayari wametuma barua kwa IGP kuhusu taarifa za tishio la kuuawa kwa Kiongozi wao, Zitto Kabwe.
Akiongea na waandishi wa habari leo kwenye ofisi za chama hiko jijini Dar es Salaam, Katibu wa Itikadi, Mawasiliano kwa Umma na Uenezi, Ado Shaibu amesema wao wamepokea taarifa hizo kutoka kwenye mitandao ya kijamii.
Katibu huyo ameongeza kuwa hawawezi kupuuzia taarifa hizo kwa kuwa mpaka leo hii bado haifahamiki Ben Saanane yuko wapi.
“Lakini tumemwandikia barua IGP ili achunguze taarifa hizo, hatuwezi kupuuza kwa sababu Chadema ililalamika kabla ya shambulio la Tundu Lissu, hatupuuzi kwa sababu, leo hii hatujui Ben Saanane yuko wapi,” amesema Katibu huyo.