Bongo5 Exclusives
African film development awards 2013 kutolewa Dar, 29 June, MC kuwa Tracy Morgan na Kerry Washington wa Marekani
Jiji la Dar es Salaam litakuwa na ugeni mkubwa mwezi June mwaka huu ambapo tuzo za maendeleo ya filamu za Afrika 2013 zitatolewa.
Tuzo hizo zitakazofanyika kwenye hoteli ya Hyatt Regency zitawatuza watu, serikali na makampuni yaliyotoa mchango mkubwa kwa maendeleo ya filamu barani Afrika. Jumla ya tuzo 30 zitatolewa kwa kutumia nominations na tuzo 6 zitatolewa kwenye vipengele visivyokuwa na nominations.
Tuzo hizo pia zitawapa heshima waigizaji wakongwe wa Marekani wenye asili ya kiafrika Morgan Freeman na Whoopie Goldberg.
Kwa taarifa zaidi tembelea http://www.theafricanfilmconsortium.org