Bongo Movie

Afrika Mashariki na Magharibi tunaongoza kwa tamthilia zenye ubora – Steve Nyerere

Msanii wa filamu Bongo, Steve Nyerere amesema tasnia hiyo kwa sasa inaongoza Afrika Mashariki na Magharibi kwa kutoa tamthilia zenye ubora.

Muigizaji huyo ameiambia Clouds Fm kuwa mafanikio hayo yamefikiwa baada ya wasanii kugundua sehemu waliyojikwaa na kuamua kuinuka na kuanza upya.

“Tumesimama sasa katika Afrika Mashariki na Magharibi yote tunaongoza kwa kuonyesha tamthilia zenye ubora, inaonyesha ni kwa kiasi gani Tanzania kuna vipaji,” amesema.

Ameongeza kuwa kilichobaki kwa sasa ni wasanii kuongeza thamani ya kazi zao na kujithamini na sio kuwa kawaida kwenye kila jambo ambalo wanafanya.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents