Afya ya Muhammad Ali yazorota zaidi
Afya ya bingwa wa ndondi wa zamani Muhammad Ali hivi karibuni imekuwa mbaya zaidi na kaka yake ameonya kuwa maisha yake yanaweza kuwa mwishoni sasa. Kaka yake huyo ameliambia gazeti la The Sun kuwa kaka yake anaweza kufariki muda si mrefu.
‘He’s in a bad way. He’s very sick. It could be months, it could be days. I don’t know if he’ll last the summer. He’s in God’s hands,’ alisema.
Mara ya mwisho Ali alionekana kwenye mashindano ya Olimpiki mwaka jana jijini London.Muhammad Ali anaumwa ugonjwa uitwao Parkinson’s ambao umekuwa ukimsumbua kwa muda na kumfanya kutetemeka muda wote.