Burudani
Afya ya Tuddy Thomas yaendelea kuimarika
Mtayarishaji wa muziki Tuddy Thomas aliyevamiwa hivi karibuni na vibaka na kukatwa mapanga akiwa nje ya maeneo ya Mlimani City jijini Dar es Salaam, anaendelea vizuri.
Tuddy amesema tayari ameshaanza kufanya mazoezi madogo madogo ili kuimarisha afya yake.
“Naendelea salama ingawa bado sijakaa vizuri, nafanya mazoezi, kwa sababu niliumia mikono yote,” Tuddy alikiambia kipindi cha XXL cha Clouds FM.
Aliongezea, “Nafikiri mpaka kufika October nitakuwa sawa, nitakuwa nimeanza kufanya kazi. Kazi ndio maisha, pia nimemiss sana kufanya kazi kwa sababu mimi napenda sana kufanya kazi.”