Habari
Aibu kwa Tanzania kuwa na chaguzi zisizokuwa huru na haki – Prof. Lipumba (+video)
Mwenyekiti wa CUF Taifa, Prof. Ibrahim Lipumba ametaka Tume ya Uchaguzi(NEC) kujirekebisha na kuhakikisha wasimamizi wa uchaguzi wanafuata sheria na kanuni za uchaguzi bila kupendelea Chama chochote, huku akieleza kuwa ni aibu kubwa kwa nchi kama Tanzania kuwa na chaguzi zisizokuwa huru za haki miaka 27 baada ya mfumo wa Vyama vingi kuanzishwa.