Airtel Yawazawadia washindi wa ‘Nani Mkali’ promosheni
Afisa mawasiliano wa Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Bi. Dangio Kaniki akimpongeza mmoja wa washindi wa shindano la Nani Mkali Bw Daniel Mshana baada ya kusaini fomu ya kuthibitisha ushindi baada ya kujishindia pesa taslimu milioni moja katika hafla iliyofanyika makao makuu ya Kampuni ya Airtel, wa pili kushoto ni washindi wengine ambao ni Bw Albogast Oiso akifatiwa na Dr.Hetal Anthan akishuhudia kulia ni Afisa Uhusiano wa Kampuni ya Airtel Bi Jane Matinde.
Mmoja wa washindi wa shindano la Mkali Nani linaloendeshwa na kampuni ya simu za mikononi ya Airtel Bw Daniel Mshana(katikati) akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) baada ya kukabidhiwa kitita cha shilingi milioni moja baada ya kuibuka kuwa mshindi wa wiki ya kwanza ya promosheni ya nani mkali. Pichani (kushoto)ni mshindi Bw Albogast Oiso (kulia) ni Afisa mawasiliano wa Airtel Bi.Dangio Kaniki akifatiwa na moja ya mshindi Dr.Hetal Anthan.