AKA ameimba kwenye ngoma aliyofanya na Diamond – Meneja
Rapper Kiernan Jordan Forbes maarufu kama AKA anapewa cheo kama rapper bora zaidi kwa sasa nchini Afrika Kusini lakini kurap sio kitu pekee anachoweza kufanya.
AKA ni producer wa muziki aliyesomea sound engineering. Uwezo wake wa kuimba pia unasikika kwenye ngoma yake, Congratulate na hivyo ukiambiwa kuwa ameimba kwenye ngoma aliyofanya na Diamond usishangae.
Kwa mujibu wa meneja wa Diamond, Salam Sharaf, rapper huyo ambaye hivi karibuni alipata mtoto wa kike, ameimba kwenye rekodi hiyo iliyofanyika May mwaka huu.
Salaam Sharaf has revealed that @akaworldwide sings too and will soon drop a song with @diamondplatnumz #MTVMAMA2015-workshop
— MTV ZA (@mtvza) July 17, 2015
Salam amesema hayo kwenye semina ya MTV MAMA iliyofanyika leo jijini Durban.