Burudani

Akothee adai Diamond na Mr Flavour ndio waliomtangaza kimataifa

Akothee amefunguka kuwa Diamond amemsaidia muziki wake kufika mbali baada ya kumsdhirikisha kwenye wimbo wa ‘Sweet Love’.

Muimbaji huyo wa Kenya amemuambia mtangazaji wa Citizen Radio katika kipindi cha Mseto, Mzazi Willy Tuva, “Nitasema kwamba imenifungulia mambo mengi, nimekubalika sana sana Tanzaniana na Afrika Mashariki kwa ujumla, hata kule Dyaspora pia kwa sababu watu wengi waliweza ku-relate na mimi. Unajua alishakuwa amekuwa International tuseme tu ukweli sio, wale walikuwa wanamfuata waweza kunigundua kupitia wimbo wetu wa ‘Sweet Love’ ambao leo umegonga views milioni nne,” amesema Akothee.

“Imefanya watu wameweza kutambua nyimbo zangu nyingine na kufufua zile zilizopita, hata nikienda show sasa hivi ninaenda kupaform zile ni nyimbo zangu za kitamb ninaimba na ninapata watu wanaperform mpaka chorus,” ameongeza.

Akothee pia amemtaja Mr Flavour amemsaidia sana kuweza kutambulika zaidi nchini nigeria. Inadaiwa kuwa Akothee alimlipa Diamond kiasi cha takriban shilingi milioni 36 za Tanzania kwa ajili ya kufanikisha kolabo hiyo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents