Burudani

Akothee afunguka tetesi za kumlipa Diamond milioni 36 kwaajili ya kolabo

Muimbaji wa Kenya, Akothee amefunguka tetesi zilizosambaa kuwa alimlipa Diamond Platnumz kiasi cha shilingi milioni mbili za Kenya ili ashiriki katika wimbo wake wa ‘Sweet Love’. Kiasi hicho ni takriban shilingi milioni 36 za Tanzania.

Akiongea katika kipindi cha runinga cha Talk Central cha K24, Akothee amekataa kuweka wazi lakini amedai kuwa fedha hiyo ni kitu kidogo kwa kuwa na kama wimbo huo usingekuwa mzuri wangeomba warudishiwe fedha yao.

“What is two million shillings? No! am not saying no but am not saying yes, am saying why 2 million. Is the song good, we don’t have to talk about price if the song is not good then if we have paid we will ask our money back,” amesema Akothee.

“And now the song is doing well let’s just talk about the song,’ ameongeza.

Mpaka sasa wimbo huo umefanikiwa kutazamwa mara 3,383,577 kwenye mtandao wa YouTube na umekuwa wimbo wa kwanza wa muimbaji huyo kutazamwa zaidi katika mtandao huo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents