Michezo
Alex Chamberlain kuwa nje ya uwanja kwa wiki kadhaa
Mchezaji wa klabu ya Arsenal Alex Oxlade Chamberlain atakuwa nnje ya uwanja kwa wiki kadhaa kutokana na jeraha la goti ,kocha wa Arsenal Arsene Wenger amesema.
Chamberlain mwenye umri wa miaka 22 alipata jeraha walipogongana na Javier Mascherano wakati wa mechi ya Jumanne ya vilabu bingwa Ulaya.
Aliondoka katika uwanja wa Emirates akiwa na magongo.
”Tulimpoteza Chamberlain siku ya jumanne.Jereha lake ni baya na litamuweka nje kwa wiki kadhaa,”alisema Wenger.