Burudani

Alex wa BBA Stargame apata ajali mbaya ya gari

Aliyekuwa mwakilishi wa Kenya kwenye shindano la Big Brother Africa Stargame Alex Mgash jana amepata ajali mbaya ya gari.

Kwa mujibu wa pacha wake, Malonza, Alex alikuwa akisafiri kwenye gari na marafiki zake watatu mapema jana asubuhi kabla ya gari lao kupata ajali hiyo likiwa kwenye mwendo kasi.

Alex alipelekwa hospitali ya St. Johns. Miongoni mwa matibabu atakayoyapata ni pamoja na kufanyiwa upasuaji wa mguu na shingo ambayo imeteguka.

Source: ghafla.co.ke

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents