Michezo
Alexis Sanchez aweka rekodi ya kufunga Hat-trick katika ligi tatu tofauti
Mshambuliaji Alexis Sanchez wa Arsenal ameweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza kupiga hat-trick katika ligi kuu tatu tofauti duniani, Serie A, La Liga na EPL.
Hat-trick yake ya kwanza ilikuwa wakati anaichezea Udenise ya Italia ambapo waliifunga Palermo mabao 7-0 katika mchezo wa ligi kuu soka nchini Italia mwaka 2011. Hat-trick ya pili ameipata akiwa na Barcelona nchini Hispania ambapo waliifunga Elche mabao 4-0.
Magoli matatu ya Sanchez ya weekend hii ni baada ya kuisadia timu yake Arsenal na kuifunga Leicester 5-2 iliyokuwa haijafungwa hata mchezo mmoja tangu kuanza kwa ligi kuu msimu huu.