Alikiba afunguka baada ya kuachia video ya wimbo Mwambie Sina ‘Sasa ni wakati rasmi wa kurudisha kwa jamii’
Baada ya kuachia video ya wimbo mpya unaokwenda kwa jina la ‘Mwambie Sina’ akiwa na kundi lake King’s Music Records, Alikiba amesema kuwa ni muda wa kurudisha kwa jamii kwa kusaidia kukuza sanaa.
Msanii huyo wa muziki nchini, Kiba amesema hayo kupitia kwa mitandao yake ya kijamii ya Twitter na Instagram.
”Sasa ni wakati rasmi wa kurudisha kwa jamii kwa kusaidia kukuza sanaa kwa kutambulisha na kuvipa support vipaji vipya kwa industry. Nawatambulisha kwenu vijana wangu Cheed, Killy, K2ga na Abdukiba kutoka record label yangu King’sMusic,” amesema Alikiba.
Sasa ni wakati rasmi wa kurudisha kwa jamii kwa kusaidia kukuza sanaa kwa kutambulisha na kuvipa support vipaji vipya kwa industry. Nawatambulisha kwenu vijana wangu Cheed, Killy, K2ga na Abdukiba kutoka record label yangu King’sMusic. #MwambieSina @kingsmusictz pic.twitter.com/CPwDlN8h8S
— Alikiba (@OfficialAliKiba) October 5, 2018
https://www.instagram.com/p/Boi84yCHd33/?taken-by=officialalikiba