Burudani

Alikiba afunguka kuhusu mkataba wake na Coastal Union ‘silipwi chochote, napenda kucheza mpira’

Alikiba amefunguka kwa mara ya kwanza kuhusu mkataba wake na klabu ya Coastal Union inayoshiriki Ligi Kuu Soka Tanzania Bara, ambapo amesema yeye halipwi chochote kwenye klabu hiyo na badala yake anaitumikia klabu hiyo kutangaza bidhaa yake ya Mofanya.

Image result for alikiba coastal union
Alikiba akiwa mazoezini

Akizungumzia mkataba wake na klabu hiyo kupitia kipindi cha XXL cha Clouds FM, Alikiba amesema “Mimi silipwi, sichezei kwa pesa, nacheza for fun napenda kucheza mpira. Vile vile nimeweza kuitangaza Coastal, nimeitangaza Mofaya zaidi. Vile vile Coastal wanaitangaza Mofaya hiyo nayo imenipa Milage sana kwangu mimi,“.

Kwa upande mwingine, Alikiba amesema yupo mbioni kuanza kuuza jezi  za Coastal Union zenye namba yake (7) na zitakuwa na saini yake.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents