Burudani
Alikiba ajitoa G Records
Baada ya kufanya kazi na G Records kwa miaka kadhaa tangu utambulisho katika industry ya bongo fleva Ali kiba jana ameamua kuachana na uongozi huo na kuamua kufanya kazi zake mwenyewe.
DJ Fetty aliandika katika blog yake kwamba alipokea sms kutoka kwa Guru (wa pili kutoka kushoto) ambaye ni C.E.O wa G records ikisema kuwa kuanzia sasa hawatakuwa na Ali Kiba kwasababu ameomba kufanya kazi zake mwenyewe na sasa watabaki na album zao mbili.