Burudani

Alikiba atunukiwa tuzo ya Nyota wa Mchezo

Ikiwa ni siku tano zimepita tangu zimepita tangu Alikiba aachie ngoma yake mpya ‘Mvumo wa Radi’ amepokea tuzo ya heshima ya Plaque inayoitwa Nyota wa Mchezo kupitia kipindi cha The Playlist cha Times FM.

Msanii huyo amepewa tuzo hiyo Jumatatu hii kutokana na mchango wake kwenye muziki na jitihadi alizipiga kupeperusha bendera ya Tanzania na kuwa inspire wasanii wengine wachanga na kuendelea kuwepo mpaka leo kwenye muziki.

Kiba amekuwa msanii wa tatu kupewa tuzo hiyo baada ya Vanessa Mdee aliyekabidhiwa mwezi January mwaka huu na Diamond aliyepewa mwezi wa tatu.

Kwa sasa video ya ngoma yake mpya ya Mvumo wa Radi ina views milioni 1.1 kwenye mtandao wa YouTube.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents