Alikiba kwa mara ya kwanza kushuka dimbani kuikabili KMC, kocha adai anaweza funga zaidi ya mabao 25
Mwanamuziki wa Bongo na mshambuliaji wa klabu ya Coastal Union ya Tanga, Alikiba leo anatarajiwa kushuka kwenye dimba la Mkwakwani jijini kuanza kibarua chake rasmi cha kuitumikia timu hiyo kwenye mchezo wao wa ligi kuu dhidi ya KMC.
Coastal ambayo imefanya vizuri kwenye michezo yake iliyo pita ya mwanzo mwa msimu wa ligi itamtumia Alikiba kwenye safu ya ushambuliaji huku wakiamini kuwa msanii huyo aliyeamua kukitumikia kipaji chake cha soka atafanya vizuri.
Katika mahojiano yake kocha wa klabu ya Coastal Union, Juma Mgunda amedai kuwa Alikiba ni mchezaji mzuri na mwenye uwezo hata wakufunga mabao 25 msimu huu.
“Mashabiki wa Coastal Union wanachotakiwa kufahamu ni kwamba timu hii imesajili wachezaji 30 na kila mchezaji anataka kucheza, hivyo muda ukifika kila mmoja ataonekana uwanjani.
“Najua wengi wanamuulizia Alikiba, niseme tu ataonekana uwanjani muda si mrefu na niwaambie ni mshambuliaji mzuri na anaweza kufunga zaidi ya mabao 25 msimu huu,” alisema Mgunda.
Mbali na uchezaji wake, Alikiba pia amewadhamini wagosi hao wa kaya Coastal Union msimu huu mwaka 2018/19 ambao mpaka sasa maendeleo yao si haba baada ya kushinda mchezo mmoja na kutoka sare mmoja na kushika nafasi ya nne kwa alama zao nne juu ya mabingwa watetezi wa ligi kuu soka Tanzania Bara Simba wenye pointi sita na michezo miwili.
Nakubal
Yap
Jah Bless
Bongo bhn
Namkuba nifundi ile kinyama
Nakukubali mkubwa kiba.
Yepi kwani….!?
Ndio kocha si ana ona kufunga ni rais tu kama kutafutana karanga…heri uzee kuliko uzembe
Mvutue na manyenjeeee🤣🤣🤣🤣 miguu yenyewe kama bata hiyooo
Huyo ni bosi wake co mchezaji wake atacheza akipata mda
labda afunge mkanda