Burudani
Aliyechepuka na Kevin Hart atua kwa mwanasheria wa Blac Chyna
Mwanamke anayedaiwa kuchepuka na muigizaji Kevin Hart, Montia Sabbag ametua kwa mwanasheri Lisa Bloom ambaye amekuwa akimwakilisha mrembo Blac Chyna katika kesi yake na Rob Kardashian.
Sabbag amemuangukia mwanasheria huyo, ili aweze kutetewa baada ya sakata la kudai atavujisha video inayomuonyesha akiwa na muigizaji huyo.
Bloom amekuwa akimtetea Blac Chyna dhidi ya Rob Kardashian na mwanadada Quantasia Sharpton anayemshutumu muimbaji Usher Raymond kumuambukiza ugonjwa wa zinaa.
Kupitia mtandao wa Twitter Bloom ameweka wazi kumtambua mrembo anayetarajia kumuwakilisha kesho katika mkutano.
“I represent the woman at the center of the Kevin Hart scandal. Press conference tomorrow,” ameandika Bloom.