Uncategorized

Aliyemtoa Arsene Wenger nchini Japan na kumpa mkataba wa kuinoa Arsenal afariki dunia

Aliyekuwa mwenyekiti wa klabu ya Arsenal kwazaidi ya miaka 30, Peter Hill-Wood amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 82.

The old Etonian also oversaw the move from Highbury to the Emirates Stadium in 2006

Hill-Wood aliingia kwenye bodi ya Arsenal mwaka 1962 na kupata nafasi ya mwenyekiti  mwaka 1982 nafasi aliyoitumikia mpaka 2013 na kuachana nayo kufuatia kuanza kusumbuliwa ugonjwa wa shinikizo la moyo.

Hill-Wood was involved in Arsenal for a total of 51 years, 31 of those as chairman of the club

Maamuzi yake ya kwanza baada ya kupata nafasi ya mwenyekiti alimuajiri  Arsene Wenger kuwa meneja wa timu hiyo mwaka 1996 akimchukua kutoka Japan, chaguo ambalo lilipingwa na watu wengi kwa wakati huo kabla ya Mfaransa huyo kuwaonyesha uwezo wake na kupata mafanikio makubwa.

Under Hill-Wood, Arsenal enjoyed their greatest season - the Invincibles campaign of 2003/04

Wakitoa taarifa ya kifo chake klabu hiyo imesema ‘’ Kwa majonzi makubwa wanatoa taarifa ya kifo cha aliyekuwa mwenyekiti wa timu hii Peter Hill-Wood,’’ imesema Arsenal.

Taarifa hiyo imeendelea ‘’Tukiwa tunasherehekea miaka 100 ya mafanikio msimu huu, familia ya Hill-Wood inapenda kuelezea tulipotoka, umoja na mabadiliko ya sasa kwenye soka la Uingereza,’’

Peter Hill-Wood, who served appointed Arsene Wenger as Arsenal manager, has died aged 82 

Mbali ya kumleta George Graham kama kocha ndani ya Arsenal lakini pia Hill-Wood aliiongoza klabu hiyo kwa mafanikio makubwa ambapo wakati wake aliweza kutwaa makombe mawili ya ligi, FA Cup, League Cup na European Cup lakini pia mabadiliko ya kuachana na matumizi ya uwanja wa Highbury hadi kuamia Emirates mwaka 2006.

He also appointed George Graham, who led the Gunners to two league titles and several cups

Wenger aliiyongoza Arsenal kuchukua mataji matatu ya Premier League, manne FA na huku ukiwemo msimu wake wa mafanikio mwaka 2003/04 ambapo aliweza kumaliza ligi hiyo bila kufungwa.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents