Burudani

Aliyetaka kumvamia Rihanna aachiwa

Mwanaume mmoja anayetambulika kwa jina, Salmiri Feratovic kutoka jijini New York City (NYC) aliyekamatwa wiki iliyopita kwa kuruka na kutaka kuingia nyumba anayoishi msanii Rihanna ameachiwa huru.

Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ, Salmir alikamatwa Jumanne iliyopita na kushtakiwa kwa kosa la kuvamia nyumba ya msanii huyo huku akiwa amekutwa na kisu na kudai kuwa kisu hicho alikuwa nacho kama kujihami.

Hata hivyo Mahakama iliamuaru mtu huyo aachiwe huru na hatimaye siku ya Jumatano mchana aliachiwa huru.

Tangu mwaka jana Samir amekuwa akitumia mitandao ya kijamii kwa kujisifia na kudai kuwa na mahausiano na wanamuziki kutokea Marekani akiwemo Nick Minaj, na Beyonce huku akidai kuwa na watoto na wasanii hao.

Kuachiwa huru kwa mwanaume huyo kunaweza kukaongeza ulinzi nyumbani kwa Rihanna, pia kunaweza kumfanya akae mbali na shabiki zake kwa kuhofia kudhuliwa.

Na Laila Sued

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents