Habari

Aliyewahi kuwa kiongozi wa juu wa kundi la Al-Shabaab ajisalimisha

Maafisa nchini Somalia wamesema aliyewahi kuwa kiongozi wa juu wa kundi la al-Shabaab, Mukhtar Robow amejisalimisha kwa majeshi ya Serikali katika mji Huddur magharibi mwa Somalia.

Mukhtar Robow

Bwana Robow alikuwa kiongozi na msemaji mkuu wa kundi la al-Shabaab kabla ya kutofautiana na kundi hilo miaka minne iliyopita.

Mwezi Juni mwaka jana 2016, Marekani iliondoa zawadi ya dola milioni tano kwa bwana Robow ambaye bado anaaminiwa kuendelea na shughuli zake kama mwanamgambo.

Al Shabab bado inadhibiti maeneo makubwa ya Somalia na kufanya mashambulizi ya mara kwa mara nchini Somalia na nchi jirani ya Kenya.

By Godfrey Mgallah

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents