Burudani

Amber Rose afuta sura ya Wiz Khalifa

Mwanamitindo Amber Rose ameonekana kuamua kuanza kumfuta kabisa ex wake Wiz Khalifa.

                                                                      Kushoto ni picha ya zamani na kulia ni muonekano wake wa sasa

Mrembo huyo ambaye amefanikiwa kupata mtoto mmoja na rapper huyo, ameamua kufuta tattoo ya Wiz ambayo aliichora katika mkono wake wa kushoto.

Amber ambaye kwa sasa ana mahusiano na rapper 21 Savage, alikuwa amechora tattoo hiyo ambayo inaonyesha sura ya mzazi mwenzake huyo na sasa amechora sura ya mwanaume mwengine ambaye bado hajafahamika.

Inadaiwa kuwa mrembo huyo aliifuta tattoo hiyo ya Wiz Ijumaa iliyopita mjini Miami Beach – Florida kwa mchoraji maarufu Sugar Factory American Brassiere.

Na Laila Sued

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents