Burudani
Amber Rose apanga kumualika Wiz Khalifa kwenye kipindi chake cha TV
Mwanamitindo maarufu asiyeishiwa vituko, Amber Rose amepanga kumualika Wiz Khalifa kwenye show yake ya ‘Amber Talk Show’.
Siku chache zilizopita Amber Rose alidai kuwa atakuwa na furaha kubwa kumkaribisha mume wake wa zamani katika kipindi hicho kwa ajili ya kuelezea maisha yake.
Kupitia akaunti yake ya Instagram, Wiz Khalifa alisema ataenda kupita tu, hatokuwa na muda wa kupoteza, lakini anashukuru sana kwa kupewa nafasi hiyo kuwa mgeni rasmi kwenye show hiyo.
Aidha wawili hao walifanikiwa kuzaa mtoto mmoja wa kiume, Sebastian (3) lakini mahusiano yao yalivunjika mwaka jana.