Burudani
Amber Rutty na James Delicious wakutwa na makosa mawili mahakamani, moja la kuingiliwa kinyume na maumbile (+video)
Msanii wa muziki Amber Rutty na mumewe leo Novemba 02, 2018 wamefikishwa katika Mahakama ya mkazi Kisutu jijini Dar Es Salaam kufuatia video yao ya utupu kuvuja mtandaoni wiki iliyopita.
Wakiwa Mahakamani hapo, wote wawili wamesomewa mashtaka mawili moja la Kuingilia/Kuingiliwa kinyume na maumbile huku lingine likiwa la kusambaza video chafu kwenye mitandao ya kijamii.
Kwa upande mwingine James Delicious naye amepandishwa kizimbani ambaye yeye amesomewa shtaka moja la kusambaza picha za ngono mtandaoni.
Watuhumiwa wote watatu wameachiwa kwa dhamana na kesi yao itasikilizwa tena Novemba 12, 2018, hii ni baada ya upande wa mashtaka kuiomba mahakama kwa ajili ya upelelezi.