Michezo
Amir Khan kuzipiga na Sauli Alvarez
Bondia Amir khan kutoka Uingereza anatarajia kupambana na bondia kutoka Mexico Sauli Alvarez kuwania mkanda wa WBC katika uzito wa kati mnamo mwezi mei saba mjini Las Vegas.
Amir khan
Khan mwenye miaka 29, ambaye ni bingwa wa dunia katika uzito wa welter hajapigana tangu apigwe na Chris Algieri mjini New York mwezi Mei.
Kwa upande wa Alvarez mwenye miaka 25, amewahi kumpiga bondia Miguel Cotto kwa pointi mjini Las Vegas mwezi Novemba.
Bondia Sauli Alvarez ambaye ndo apambana na Amir khan
Mpaka sasa amepoteza pambano mara moja huku akishinda mara 46 katika mapambano yake