Burudani

Anayedai kuambukizwa ugonjwa na Usher Raymond atema cheche

Mwanadada Quantasia Sharpton, anayedai kuambukizwa ugonjwa wa zinaa na mwanamuziki Usher Raymond amezidi kuandamwa na mitandao kuwa anachokifanya kwa msanii huyo ni kutafuta fedha.

Kauli za watu zimekuja baada ya kunaswa kwa post yake kwenye mtandao inayosemeka kuwa anahitaji fedha tu, hata hivyo imekanushwa kuwa kesi hiyo haihusiani na kasi aliyoifungua dhidi ya mwanamuziki huyo.

Kwa mujibu wa mwanasheria wake Lisa Bloom ameueleza mtandao wa TMZ, kuwa mteja wake aliandika maneno hayo kabla hata ya kesi yao kupamba moto, pia mrembo huyo ni mtu kama watu wengine nchini humo wanaokuwa na huitaji wa pesa. Vile vile Bloom amewataka watu kuacha kuunganisha matukio kwani anachohitaji mteja wake ni baraza la maamuzi kutenda haki.

“It’s not a crime to be poor in America. It’s not a crime to be honest about the fact you need money. Most people need money.” She points out Quantasia didn’t put a dollar amount on the lawsuit, and only wants what a jury deems fair,” amesema Bloom.

Na Laila Sued

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents