Michezo
Andy Murray kuiongoza Uingereza kwenye Davis Cup
Mcheza tenisi, Andy Murray anayeshika namba mbili ya ubora ulimwenguni anatarajia kuiongoza Uingereza katika mchezo dhidi ya Japan katika mashindano ya Davis Cup ikiwa ni mchezo wa raundi ya kwanza kuweza kushinda mjini Birmingham kuanzia tarehe 4-6 mwezi March.
Murray mwenye miaka 28 ataungana na Jamie , Kyle Edmund, Dominic Inglot pamoja na Dan Evans. Uingereza ilishinda katika mashindano ya Davis Cup mara ya kwanza mwaka 1936 dhidi ya Ubelgiji.