Michezo
Antonio Conte kama akitua Chelsea anakuja na mbadala wa John Terry
Klabu ya Chelsea kama itafanikiwa kumpata kocha, Antonio Conte yu tayari kuja na beki wa kuziba nafasi ya nahodha wa Chelsea, John Terry kwa kufanikisha uhamisho wa staa wa Juventus, Leonardo Bonucci.
Kwa mujibu wa mtandao wa Tuttomercatoweb wa Italia, kocha huyo wa kikosi cha Italia, ameliweka nafasi ya juu jina la beki huyo katika orodha ya mastaa anaotazamia kuziba nafasi ya nahodha huyo.
Conte alifanya kazi na Bonucci katika kikosi cha Italia na wakati alipokuwa kocha wa Juventus na wawili hao wana urafiki wa karibu.