Argentina yabanwa mbavu na Iceland, Lionel Messi akosa penati
Timu ya taifa ya Argentina imeshindwa kutamba mbele ya Iceland baada ya kulazimishwa sare ya bao 1 – 1 kwenye mchezo wa kombe la dunia huko Urusi licha ya kuwa na wachezaji wenye majina makubwa ndani ya kikosi chake.
Dakika ya 19 ya kipindi cha kwanza, Sergio Aguero alianza kuifungia Argentina bao la kuongoza kabla ya kusawazishwa na mchezaji wa Iceland, Finnbogason dakika ya 23.
Katika hali isiyotarajiwa mshambuliaji wa timu ya taifa ya Argentina na klabu ya Barcelona, Lionel Messi amekosa mkwaju wa penati dakika ya 64 ya mchezo jambo ambalo limewashangaza wengi.
Kikosi cha Argentina: Halldorsson, Saevarsson, Sigurdsson, Arnason, Magnusson, Gudmundsson, Bjarnason, Gunnarsson, Hallfredsson, Sigurdsson, Finnbogason
Waliyokuwa benchi: Schram, Runarsson, Ingason, Eyjolfsson, Skulason, Fridjonsson, Gudmundsson, Skulason, Traustason, Sigurdarson, Gislason, Bodvarsson
Kikosi cha Iceland: Caballero, Tagliafico, Rojo, Otamendi, Salvio, Biglia, Di Maria, Meza, Mascherano, Messi, Aguero
Waliyokuwa benchi: Guzman, Armani, Mercado, Ansaldi, Fazio, Banega, Acuna, Perez, Lo Celso, Higuain, Dybala, Pavon