Arnold Schwarzenegger amesema kuwa hatomfungulia mashtaka mtu aliyemshambulia kwa kumpiga teke katika moja ya hafla nchini Afrika Kusini (+ Video)
Arnold Schwarzenegger amesema kuwa hatomfungulia mashtaka mtu aliyemshambulia kwa kumpiga teke katika moja ya hafla nchini Afrika Kusini (+ Video)
Nyota wa Hollywood Arnold Schwarzenegger amesema kuwa hatomfungulia mashtaka mtu aliyemshambulia katika hafla moja nchini Afrika Kusini. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 71 alikuwa akizungumza na mashabiki katika hafla yake ya Arnold Classic Africa sporting event iku ya Jumamosi wakati mtu alipomrukia na kumpiga teke mgongoni.
Kwa mujibu wa BBC. Mshambuliaji huyo baadaye alikamatwa na kuzuiwa. Hatahivyo siku ya Jumapili , Schwarzenegger alisema kwamba hatomchukulia hatua mtu aliyemshambulia akisema tukio hilo limepitwa na wakati.
And if you have to share the video (I get it), pick a blurry one without whatever he was yelling so he doesn’t get the spotlight.
By the way… block or charge? pic.twitter.com/TEmFRCZPEA
— Arnold (@Schwarzenegger) May 18, 2019
Kanda hiyo ya video ,iliosamabazwa katika mitandao ya kijamii ilimuonyesha Schwarzenegger akipiga picha na mashabiki wake wakati mtu aliyemshambulia alipotoka nyuma na kupiga flying kick.
Nyota huyo wa filamu ya Terminator aliteteleka karibu aanguke huku mshambuliaji akianguka ardhini ambapo anakamatwa na walinzi mara moja.
Mtu huyo ambaye jina lake halikutajwa baadaye alikabidhiwa maafisa wa polisi, kulingana na maafisa wa hafla hiyo.
Schwarzenegger alituma ujumbe wa twitter kwa zaidi ya mashabiki wake milioni nne: Nilidhania kwamba nilikuwa nimesukumwa na watu waliojaa katika hafla hii , ambacho ni kitu cha kawaida.
Niligundua kwamba nilipigwa teke nilipoona kanda ya video kama vile nyinyi. Akijibu ujumbe wa twitter kutoka kwa mashabiki wake siku ya Jumapili, alisema kwamba hatomfungulia mashtaka mashambuliaji wake.
Update: A lot of you have asked, but I’m not pressing charges. I hope this was a wake-up call, and he gets his life on the right track. But I’m moving on and I’d rather focus on the thousands of great athletes I met at @ArnoldSports Africa.
— Arnold (@Schwarzenegger) May 19, 2019
”Tuna michezo 90 hapa Afrika Kusini na wanamichezo 24,000 wa kila umri-kitu kinachotupatia moyo kushiriki.Tuwaangazie wanariadha hawa”, aliandika katika mtandao wake wa Twitter.
Hafla hiyo ya michezo ya Arnold Classic Afrika hufanyika kila mwezi Mei na hushirikisha michezo kadhaa ikiwemo ujengaji misuli na michezo ya kukabiliana