Michezo
Arsenal yavuliwa ubingwa Kombe la FA, Man United yatoka sare na West Ham
Michuano ya kombe la FA iliendelea tena jana kwa mabingwa wake Arsenal kuvuliwa ubingwa baada ya kufungwa na Watford kwa mabao 2-1.
Magoli ya Watford yalifungwa na Odion Ighalo na Adlene Guedioura huku bao la kufutia machozi la Arsenal likifungwa na Danny Welbeck.
Katika mchezo mwingine Manchester United walitoka sare na West Ham united ya bao 1-1.
Goli la West Ham lilifungwa na mchezaji Dimitri Payet dakika ya 68 kipindi cha pili, huku bao la kusawazisha la Manchester United likipachikwa na Anthon Martial Dakika ya 83 kipindi cha pili