Michezo

Arsene Wenger aichomolea Fulham dakika za mwisho kabla ya kutangazwa Claudio Ranieri

Aliyekuwa meneja wa Arsenal, Arsene Wenger amekataa nafasi ya kurithi mikoba ya kocha Slavisa Jokanovic ndani ya klabu ya Fulham inayoshiriki ligi ya kuu Uingereza.

Arsene Wenger turned down the chance to replace Slavisa Jokanovic as Fulham manager

Aliyekuwa kocha wa Arsenal, Arsene Wenger 

Kwa mujibu wa Daily Telegraph, mmiliki wa klabu ya Fulham, Shahid Khan wiki iliyopita alizungumza na wagombea wa nafasi ya kuifundisha timu hiyo huku jina la Wenger likipendekezwa kabla ya kumteua Claudio Ranieri.

Claudio Ranieri has replaced Jokanovic as boss of Fulham after a difficult start to the season

Kocha wa Fulham, Claudio Ranieri ambaye amechukua nafasi ya Jokanovic

Lakini Mfaransa huyo alikataa na kusisitiza kuwa kamwe hatakuwa tayari kuzifundisha klabu za Uingereza baada ya kuzifundisha kwa takribani miaka 22 akiwa Arsenal na kufanya hivyo ni kuishushia heshima The Gunners.

Fulham kwa sasa inashika mkia kwenye msimamo wa ligi hiyo baada ya kuwa na pointi tano pekee mpaka sasa.

Hii siyo mara ya kwanza kwa Mzee Wenger kuhusishwa kurejea kwenye soka kwani alishawahi kuzungumzwa kutua Real Madrid ambaye kwa sasa imemtangaza Santiago Solari kama kocha mkuu.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents