Michezo
Arturo Vidal afukuzwa na kocha wa timu ya taifa ya Chile kwa ulevi
Mchezaji wa timu ya taifa ya Chile na klabu ya Bayern Munich ya Ujerumani, Arturo Vidal amefukuzwa na kocha wake, Jorge Sampaoli.
Timu ya taifa ya Chile ipo kwenye maandalizi ya kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya Paraguay. Wachezaji wote wapo kambini na wanaendelea na mazoezi lakini Vidal aliripoti kwenye kambi ya timu ya hiyo Jumanne mchana akiwa amelewa.
Kocha wake hakupendezwa na kitendo hicho na alimrudisha kwa kumwambia arudi Ujerumani hadi pale atakapokuwa tayari.
Kocha huyo pia alimpa onyo kali na amempa nafasi ya mwisho.