Michezo
Asamoah Gyan ashindwa kujiunga na klabu ya Reading
Nahodha wa Ghana Asamoah Gyan ameshindwa kujiunga na klabu ya Reading inayoshiriki ligi daraja la kwanza (Championship) kwa mkopo wa muda mrefu.
Mchezaji huyo wa zamani wa klabu ya Sunderland alitarajiwa kujiunga na The Royals akitokea klabu ya Shanghai SIPG ya nchini China.
Kwa mujibu wa BBC, Gyan, 30, hataweza tena kujiunga na klabu hiyo baada ya ripoti kutoka kwamba amefeli vipimo vya afya.