ATCL waahidi kutoa tamko baada ya tuhuma kuwa shirika hilo linauza tiketi za watu waliochelewa Ndege
Shirika la Ndege la ATCL limesema kuwa litatolea maelezo kuhusu tuhuma zilizotolewa na msanii wa muziki Diamond Platnumz akidai kuwa Wafanyakazi wa shirika hilo wanauza tiketi za watu waliochelewa ndege.
ATCL wameahidi kuwa leo Desemba 17, 2018 watatoa taarifa zaidi kuhusu tuhuma hizo ambazo zimeanza kusambaa mitandao toka jana.
With great sadness Air Tanzania has received allegations that have been spreading on social media platforms. Therefore we will issue a statement on news media and our social media accounts today at 01:00 pm.
Thank You
Tazama video hiyo ambayo imesambaa mitandaoni ikimuonesha Diamond Platnumz akijibizana na wafanyakazi wa ATCL.
Hiki ndicho alichokutana nacho @diamondplatnumz akitokea Mwanza kwenye tamasha la Wasafi Festival..Msikilize kwa makini pic.twitter.com/uUXE417mqB
— bongo5.com (@bongofive) December 16, 2018