Burudani

Audio: Jinsi Chidi Benz na Cassim walivyowashiana Club Billicanas

Kuna sababu kubwa kwanini Bongo5 haikuandika habari iliyodai kuwa Nay wa Mitego na Chidi Benz wamepatanishwa na Cassim Mganga na sasa ni amani tu. Kilichotokea sasa ni kwamba, Chidi Benz anamuita Cassim Mganga Mchawi, kauli ambayo ambayo iliwafanya hivi karibuni watukanane matusi ya nguoni Club Billicanas, na kama wasingekuwepo watu waliowazuia, wangetoana meno siku hiyo.

IMG_9071

“Mwacheni asinizingue mimi, nakosea mimi kila siku,” anasikikia Cassim akiongea kwenye audio iliyorekodiwa na kuifikia mikono ya Soudy Brown wa U Heard. “Mimi nimekosea nini Benz apige was**ge wengine mimi hawezi kunifanya lolote, msimshike, aniguse halafu aone. Mimi si maisha yangu, nahangaika nafanya muziki wangu wanasema mimi mchawi, mimi nina familia yangu, mimi sio mchawi, namroga nini mimi, yeye stress zake, anavuta unga, mimi namsingizia? Kila mtu anajua, yeye si life yake amechagua? Asinizingue, mimi mwanaume power kama yeye.”

Sikiliza mwenyewe hapa.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents