HabariUncategorized

Audio: Mtangazaji ajifungua ‘live’ akitangaza redioni

Duniani kuna mengi yanatokea na kushangaza, huku mengine yakikuacha mdoma wazi. Mtangazaji wa kipindi cha Alfajiri katika kituo cha radio cha The Arch kilichopo katika mji wa St Louis nchini Marekani, Cassiday Proctor amejifungua mtoto wiki hii kwenye kipindi chake.

Mtangazaji huyo alipata bahati hiyo baada ya kituo chake cha habari kiliposhirikiana na hospitali ambayo alijifungua ili matangazo yake yaweze kuruka moja kwa moja hewani wakati akijifungu.

Baada ya kujifungua huku akisikika moja kwa moja radion, Cassiday amesema yeye huwaambia kila kitu wasikilizaji kuhusu maisha yake.

Mtoto huyo ambaye amepewa jina la Jameson, amezaliwa akiwa na uzito wa kilogram 3.345. Hapa chini ni sauti ya mtangazaji Cassiday wakati akijifungua akiwa hewani.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents