Audio: Shaa asema na baba wenye nyumba ‘wanoko’ kwenye Baba Kodi
Asilimia kubwa ya wananchi huanza maisha kwa kupanga kwenye nyumba ambapo kutokana na uwezo wa kila mpangaji, wapo wanaopanga kwenye chumba kimoja, viwili nk na wengine wakichukua nyumba nzima.
Kwa bahati mbaya wapangaji wengine wamejikuta wakipanga kwenye nyumba za wamiliki wasumbufu na wanoko ambao hudai pesa yao ya pango kwa usumbufu mkubwa na hao ndio Shaa ameamua kuwapa ujumbe wao kwenye Baba Kodi.
Kwa wapangaji wenye vifua vipana Baba Kodi ni wimbo mzuri kuupiga kwa sauti ili baba/mama mwenye nyumba mwenye tabia hii aweze kuupata ujumbe. Ni wimbo ambao pamoja na kuwa na ujumbe mzuri, unachezeka pia na kuufanya uwe 100% club banger.
Wimbo umetengenezwa na Manecky wa AM Records. Enjoy.