Burudani

Aunty Ezekiel afunguka kuhusu mimba yake

Zile tetesi za muigizaji wa filamu nchini Aunty Ezekiel ni mjamzito huenda zikawa zimetimia baada ya kuficha kwa muda mrefu.

Akiongea kwenye kipindi cha FNL cha EATV, Aunty hajaweka wazi kama ni kweli ni mjamzito ila alichokisema ni kuwa anatamani tena kupata mtoto mwingine wa kike baada ya mtoto wao wa kwanza Cookie naye kuwa wa kike.

“I wish nipate mtoto wa kike tena, watoto wa kike hela ile, yaani mpaka wajae,” amesema muigizaji huyo.

Aunty Ezekiel ameongeza kuwa hataki kuweka wazi kama ni mjamzito kwa sasa ila watu watafahamu tu kwa kuwa hata mimba yake ya kwanza aliificha lakini watu waliweza kuibaini.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents