Michezo
Australian Open: Andy Murray adai joto la (42C) la Melbourne litaua mtu
Mchezaji wa tennis wa Uingereza, Andy Murray amesema anaogopa kuwa mtu anaweza kupata mshtuko wa moyo kama waandaji wa mashindano ya Australian Open wataendelea kusisitiza kuendelea kwa michezo kwenye joto kali la (42C) jijini Melbourne, kama walivyocheza jana Jumanne.
Murray alitumia saa 1 na dakika 27 jana na kumshinda Mjapan Go Soeda kw a6-1, 6-1, 6-3 katika siku ambayo mchezaji wa Canada, Frank Dancevic alizimia akiwa mchezoni dhidi ya Peng Shuai wa China, aliyetapika.
Frank Dancevic akipewa huduma ya kwanza baada ya kuanguka uwanjani kutokana na joto kali
Kijana anayechukua mipira naye alianguka wakati wa mechi nyingine
Bingwa huyo wa Wimbledon alisema uamuzi wa kuruhusu michezo iendelee inaonesha picha mbaya ya mchezo huyo.