Burudani
Avril akiri Ay kumwingiza kwenye muziki
Mwanamuziki Avril alijikuta akitamka juu ya uweli wake wa kuingia kwenye gemu la Muziki, baada ya kufurahia kufika Tanzania na kufanya Show ya miaka 50 ya Uhuru, katika viwanja vya Mbaramwezi Beach siku ya 9 Dec.
Avril kutoka Kenya amesema kwamba mwanamuziki Ambwene Yesaya Ay ndiyo aliyemshawishi kuingia kwenye muziki huo, na ndiyo maana leo ametoa shukrani zake za wazi na kuvutiwa mila ya kikwazo kwa mwana kaka huyo wa Bongo.
Pia amesema amevutiwa sana na Wanzania kwa kudumisha Amani miaka 50, ila zaidi ni kufanya Show kwake kwa mara ya kwanza nchini Tanzania.
Ila kwa mashabiki ikawa patashika nguo kuchanika, kila mmoja anatamani amshike na kumgusa hii kutokana na dada huyo kuwa na mvuto na kivazi chake alichopandia stejini.