Burudani
Ay na Fa kuwasha moto Maisha Club
mwanamuziki Hamisi Mwijuma ‘Mwana Fa’ na Ambwene Yesaya ‘Ay’ wanatarajia kuwasha moto wa nguvu katika tamasha la X BONGO NITE, pale New Maisha Club katika LEVO za JUU. Fa anasema si la kukosa kwani usiku huo wa mach 20 juma pili, ni wa pekee kwani wanataraji kufanya makubwa, ambayo kwa muda mrefu walikuwa hawajayafanya katika matamasha yao.
Ay na Mwana Fa hivi sasa ndiyo wasanii wanaofanya vizuri kutokana na nyimbo zao hasa nyingi kati ya nyimbo hizo kuchezeka katika Night Club, wanasema nyumbani utabaki wewe lakini wenzako wote wapo X BONGO NITE, pale New Maisha Club